Thursday, 22 January 2015

Bonanza la Vijana - Bagamoyo 21 feb 2015







Uongozi wa vijana usharika wa kurasini unayo furaha kuwataarifu vijana wote kua tutakua na bonanza la michezo la vijana wote wa usharika wa kurasini mnamo tarehe 21 february 2015 mjini bagamoyo.

Bonanza hili litaambata na semina ya vijana pamoja na kufanya utalii wa ndani katika maeneo ya kihistoria ya kaole ruins.

Ili kushiriki, kila kijana anahitajika kuchangia Tsh Elfu Ishirini na tano tu (TZS 25,000) ikiwa ni gharama za usafiri, chakula, kiingilio na vifaa vya michezo.

Kwa wale watakaopenda kupatiwa form ili kuweza kuchangisha fedha hizi wanaombwa wamuone Kiongozi yeyote wa umoja wa vijana au kumpigia simu mwenyekiti (elly- 0715 384 862).

Kwa wale ambao hawatahitaji form na wapo tayari kuchangia fedha hizo wao wenyewe, wamuone mtunza hazina wa umoja wa vijana au kiongozi yeyote na kumkabidhi fedha hizo. Hakikisha umeandikwa jina lako na kiasi ulichotoa.

Mwisho wa kukusanya michango itakua jumapili ya tarehe 15 feb 2015.


Mungu awabariki nyote.

R.I.P Julieth Mbwambo

Mnamo tarehe 8 Jan 2015 Usharika wa kurasini tulimpoteza ndugu yetu,mwana kwaya mwenzetu, bibi yetu Julieth Mbwambo.

Kwa niaba ya uongozi wa vijana usharika wa kurasini, Kwa simanzi nyingi sana tunatoa salamu za rambi rambi kwa familia yake, kwaya kuu pamoja na usharika wa kurasini kwa ujumla kwa kuondokewa na mwenzetu.

Bwana ametoa na bwana ametwaa, Jina la bwana libarikiwe.

M/kiti
Elly Emmanuel